About

About
Hii ni tovuti ya kitanzania inayoendeshea shughuli zake nchini Tanzania chini ya usimamizi wa NGOMBOZI MEDIA COMPANY . Tovuti hii inakupa fursa ya kujua na kupakua nyimbo mpya na za zamani za Bongo flava, India, pamoja na Filamu . Yapo mengi kuhusu burudani kwa ujumla utakapotembelea www.ngombozi.com . Haiishii hapo tovuti hii kadri siku zinavyozidi kusonga mbele ndio inazidi kuboresha huduma zake na kuzisogeza karibu. Imani ya wengi inawapelekea kuamini kuwa umakini unaoonyesha hivi sasa na timu ya usimamizi wa tovuti hii utaifanya izidi kuwa maarufu huku ikisogeza huduma karibu na wateja hasa wapenda burudani ya muziki wanaopendelea sana matumizi ya mtandao. Kwa ufupi kabisa hiyo ndiyo Ngombozi media Tovuti ya muziki inayoendeshea huduma zake nchini Tanzania.

Dont Miss

Hii Ndio Sababu Ya Kutofunuliwa Mwili Wa Edward Lowassa

Hii Ndio Sababu Ya Kutofunuliwa Mwili Wa Edward Lowassa
Share it:

Kupitia Ibada Maalum ya Kumwombea aliyekuwa Waziri Mkuu Mh. Hayati Edward Lowassa, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Alex Malasusa, Azungumzia Utamaduni wa Kuaga Mwili.

Katika ibada maalum ya kumuombea marehemu Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu, iliyofanyika leo Februari 14, 2024, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Alex Malasusa, ametoa msimamo kuhusu utamaduni wa kuaga mwili. Malasusa amesisitiza kwamba hakuna ulazima kwa kanisa kufungua jeneza ili waumini waone mwili wa mwanadamu aliyefariki, akibainisha kuwa hiyo siyo sheria wala taratibu za kanisa.

“Tuwe tunatazamana tukiwa hai tusisubiri mtu amelala. Msifikiri kwenda kuaga lazima ufungue jeneza mtu wamuone; siyo lazima,” alisema Malasusa.

Kauli hii imetolewa leo tarehe 14/2/ katika ibada ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Edward Lowassa, aliyefariki dunia Februari 10, 2024, kauli ikilenga kuhamasisha umuhimu wa kuthaminiana na kushirikiana katika uhai badala ya kusubiri hadi mtu amefariki. Malasusa ametumia fursa hii kutoa wito kwa waumini na jamii kwa ujumla, kudumisha upendo na mshikamano wakati wote.


Share it:

Fresh Air

NEWS

Post A Comment:

0 comments: