Breaking News

Atumia Saa 1:30 Kupanda Jengo La Ghorofa 101

Atumia Saa 1:30 Kupanda Jengo La Ghorofa 101

Mpanda majengo marefu na miamba hatari maarufu

wa Marekani, Alex Honnold, amefanikiwa kupanda jengo refu la

ghorofa 101 jijini Taipei, Taiwan, bila kutumia kamba, mkanda wa

usalama wala vifaa vyovyote vya kujilinda.

Jengo hilo lijulikanalo kama Taipei 101 lina urefu wa mita 508 na

limejengwa kwa chuma, kioo na zege, likiwa na muundo

unaofanana na shina la mianzi, jengo hili ndilo lililoshikilia kuwa

jengo refu zaidi duniani kwa mwaka 2004 hadi 2009 ambapo

sasa linashikilia nafasi ya 11 duniani na ndilo jengo refu zaidi

Taiwan likishika nafasi ya kwanza.

Honnold, anayejulikana duniani kwa kupanda miamba kwa

mtindo hatari wa free solo, aliweka historia hapo awali kwa

kuwa mtu wa kwanza kupanda jabali la El Capitan lenye urefu

wa mita 915 katika Hifadhi ya Taifa ya Yosemite, California, bila

kamba wala vifaa vya usalama na kupelekea kushinda tuzo ya

Oscar.

Safari yake ya kupanda Taipei 101 ilikuwa imepangwa kufanyika

Jumamosi, lakini ilicheleweshwa kutokana na mvua.

Upandaji huo ulirushwa mubashara na Netflix, ambayo ilisema

kulikuwa na ucheleweshaji mdogo wa matangazo ili kuzuia

kuonyesha tukio lolote baya endapo lingetokea "Tungekatisha

matangazo," alisema mmoja wa wakuu wa Netflix, Jeff Gaspin,

akinukuliwa na jarida la Variety kabla ya tukio hilo na kuongeza

kuwa "Hakuna anayetarajia wala kutamani kuona jambo baya

likitokea."

Honnold alikamilisha upandaji huo kwa muda wa saa moja na

dakika 31 siku ya Jumapili Januari 25, akivunja rekodi ya awali

kwa zaidi ya nusu ya Mfaransa Alain Robert, anayejitambulisha

kama "Spiderman", ndiye aliyewahi kupanda jengo hilo hapo

awali kwa saa nne, akitumia kamba na mkanda wa usalama.

Makamu wa Rais wa Taiwan, Hsiao Bi-khim, alimpongeza

Honnold kupitia mtandao wa X akisema, "Nakiri, ningejisikia

kichefuchefu pia, hata kuangalia ilikuwa vigumu" Honnold

alikaribishwa juu ya jengo hilo na mke wake, ambaye alieleza

kuhusu upepo na joto wakati wa upandaji.

No comments